Hisapepe Kituo Cha Msaada - Maswali Ya Mara Kwa Mara ya Wanachama
SUBIRI! TAFADHALI IELEWE KWANZA HISAPEPE KABLA HUJAENDELEA...HISAPEPE NI NINI?
hisapepe.com ni tovuti ya kawaida kabisa kama yoyote uijuayo. Ukiwa Yahoo! kwa mfano huwa unaona matangazo na unaweza kupokea barua pepe toka kwao zikikuelezea huduma zao. Matanngazo uyaonayo ukiwa yahoo yamelipiwa na wadhamini, Yahoo! inatengeneza pesa toka kwa hawa wafadhili na wanatumia pesa hiyo kukupatia wewe huduma ya bure kabisa ya barua pepe. Ni mtindo wa faida kwa wewe na wao kwa kuwa bila wewe wasingepata hayo matangazo na bila hayo matangazo wewe usingepata hiyo huduma ya bure ya barua pepe. Hisapepe.com imesimamia karibu jukwaa la mtindo huo huo ila pesa toka kwa wadhamini/watangazaji wetu badala ya kukupatia huduma ya bure ya barua pepe tunakupatia fedha hii wewe mwanachama. TUNAWATOZA WADHAMINI/WATANGAZAJI NA KUGAWANA MAPATO NA WEWE. HAKUNA CHA ZAIDI. Utapokea matangazo unayochagua na pia utashiriki kujaza dodoso (questionnaires) za utafiti mbalimbali na tutakulipa kwa hayo yote kadiri tunavyowatoza watangazaji/watafiti/wadhamini.
|
|
- Hisapepe.com inapatikana katika lugha ngapi?
- Hisapepe.com ina lugha mbili, Kiingereza na pia inapatikana kwa Kiswahili kwa wanaopendelea Kiswahili. Kupata Kiswahili bonyeza bendera ya Tanzania au nenda http://www.hisapepe.com/pages/swahili. Kurudi Kiingereza bonyeza bendera ya Marekani (tumetumia kiingereza cha kimarekani)
- Ninaishi nje ya Tanzania, naruhusiwa kujiunga?
- Ndiyo, tunawakaribisha msio Tanzania ila huenda kusiwe na mengi yatayotumwa kwenu kama itakavyokuwa kwa walio nchini. Kabla hujajiunga fikiria pia ni vipi tutakulipa. Tunashauri mlio nje ya nchi mchague “Advertising Method” yaani utakacholipwa hapa hisapepe.com utakitumia kama malipo ya wewe kuweka matangazo yako (redemption). .
- Wakenya na Waganda majirani zetu, mmetujali pia?
- Wapendwa majirani zetu wa Kenya na Uganda tunaweza kuwalipa ila mngesubiri kidogo tumalize suala la kimamlaka zaidi, tukiwa tayari tutaainisha katika ukurasa wa masharti yetu, mipango inasukwa ili tuweze kuwafikia kwa mitandao ya Zain/Celtel, MTN, Orange,Warid na Safaricom, na ikiwa tayari tutasema, tafadhali changua “Advertising Method” ili utumie pesa yako kuweka matangazo yako. Angalia pia M-Pesa imeandikwa M-Pesa-Tz kwa kuwa haiwezekani M-Pesa ya Tanzania kumlipa mteja wa M-Pesa ya Kenya. Pia njia nyingine kama PayPal n.k zinawajia punde! .
- Hisapepe kama kampuni yenyewe inapataje pesa?
- hisapepe.com ni tovuti ya kawaida kabisa kama yoyote uijuayo. Ukiwa Yahoo! kwa mfano huwa unaona matangazo na unaweza kupokea barua pepe toka kwao zikikuelezea huduma zao. Matanngazo uyaonayo ukiwa yahoo yamelipiwa na wadhamini, Yahoo! inatengeneza pesa toka kwa hawa wafadhili na wanatumia pesa hiyo kukupatia wewe huduma ya bure kabisa ya barua pepe. Ni mtindo wa faida kwa wewe na wao kwa kuwa bila wewe wasingepata hayo matangazo na bila hayo matangazo wewe usingepata hiyo huduma ya bure ya barua pepe. Hisapepe.com imesimamia karibu jukwaa la mtindo huo huo ila pesa toka kwa wadhamini/watangazaji wetu badala ya kukupatia huduma ya bure ya barua pepe tunakupatia fedha hii wewe mwanachama.
- Inafanyaje kazi? Ninapataje pesa kwa kuangalia tu matangazo?
- hisapepe.com imetengenezwa kwa program ya kompyuta yenye teknolojia ya hali ya juu sana inayosimamia na kuendesha akaunti zote na matangazo yote yaliyo hisapape.com. Program hii inachofanya ni kubandika matangazo na kukutumia baadhi katika anuani ya barua pepe yako. Kila tangazo ambalo unalipwa likitumwa kwako ama likiwekwa katika tovuti ya hisapepe basi huwa na na anuani ya siri nyuma yake ambapo ukisoma tangazo hilo basi moja kwa moja akaunti ya mdhamini/mtangazaji inakatwa Salio na linahamia kwako, kiasi hutegemea na tangazo hilo linalipiwa Tsh ngapi na makato ya gharama hisaepe imeingia. Hivi ndivyo unavyojipatia pesa na hivi ndivyo hisapepe.com inavyoweza kufidia gharama zake.
- Kuna njia ngapi tofauti za kupata pesa nikiwa hisapepe?
- Zipo njia nyingi na nyingine nyingi zinakuja, kwa sasa unaweza kupata pesa kwa:
Kupokea Barua Pepe Za Matangazo (inbox): Lipwa Kwa Kupokea Na Kusoma Barua Pepe Za Matangazo, hii italeta tangazo katika sanduku lako la barua pepe (email inbox) na nakala pia katika sanduku lako la baruapepe la hisapepe. Uliwahi kudhani email yako inaweza kuja kuwa na manufaa namna hii?
Lipwa Kubofya : Utalipwa Kwa Kubofya na Kusoma Matangazo, utaona mabango mbalimbali ya matangazo katika hisapepe.com, kazi ni moja tu, kubonyeza(bofya) matangazo hayo yatafunguka na unapolisoma sisi tunakupatia pesa yako.
Lipwa Kujiunga : Utalipwa Kwa Kujiunga Na Mitandao Au Ofa, au tovuti mbalimbali, wenye bidhaa hizi wametenga pesa za kulipia kupata wanachama wapya. Hisapepe inakupatia fedha hizo ujiunge na tovuti zao.
Lipwa Kusafu: Utalipwa Kwa Kusafu (Surf) Matangazo ya Wenzio ambao nao ni wanachama ila wana mambo/biashara wanataka kutangaza kwa wanachama wenzao. Unaposafu matangazo yao unalipwa nao wanalipia.
Lipwa Kupitia : Utalipwa Kwa Kufanya Mapitio/Review ya Matangazo ama Tovuti. Lipwa Kwa Kupiga Kura. Kuna wakati watangazaji au wanamasoko wangependa kufanya mapitio ya kazi/bidhaa/tovuti kabla ya kupelekwa sokoni, hii itawajulisha wateja wanaionaje bidhaa hiyo. Hii inaweza kuwa kama kura ama uthaminishaji, hisapepe itawatoza watangazaji nawe utapata malipo kwa kuthaminisha, kupigia kura n.k Si biahsara tu, hata tabiri kama kura za maoni, mfano, nani atakuwa Raisi nwaka fulani.
Lipwa Kutafiti : Utalipwa Kwa Kushiriki Tafiti . Jaza dodoso (Surveys and Questionnaires)na Ulipwe . Hakikisha unajibu maswali hayo mpaka mwisho usikatishe ili ulipwe. Huenda hii ni sehemu itakayokupatia salio kwa wingi zaidi kwa mara moja.
Lipwa Kualika: Huenda hii ni sehemu inayovutia kuliko zote za hisapepe. Utalipwa Kwa Kualika Wengine Wajiunge Hisapepe. Utapata Asilimia ya Mapato Yao. Unaweza ita kamisheni. Yaani kila unayemwalika ataorodheshwa katika idadi ya uliowaalika na kila pesa atakayopata (inayoplelekea mwalikaji apate gawio) nawe utaipata pia (angalia ualikaji na namna unavyofanyika). Tafadhali alika watu unaowajua tu usitume mialiko kwa usiowafahamu. Ni kinyume cha sheria na Mashati Ya Huduma ya Hisapepe.com. Ukiripotiwa akaunti yako itasitishwa mara moja.
Lipwa Kuchati: Unachat na wenzako na ikitokea kuna tangazo unapata pesa kwa kusoma tangazo hilo lililo katika chumba cha chat
- Nnaweza kupata pesa kiasi gani kwa kujiunga hisapepe?
- Mtindo tunaotumia sisi ni ule wa kama kibarua vile, yani usipofanya kazi hutopata kitu. Kiasi gani unaweza kupata inatenemea sana na kiasi gani unashiriki, matangazo mangapi unasoma na jinsi unavyojituma katika tafiti (surveys), mapitio (reviews) na kufungua matangazo mengi iwezekanavyo. Utaona salio la akaunti yako likiongezeka kila mara unapofanya kitu.
- Mara ngapi naweza kubadili neno langi la siri (password?)
- Hakuna kipingamizi cha mara ngapi unaweza kubadili. Hata hivyo hatukushauro kubadili badili kila mara, kubadilibadili kunaongeza uwezekano wa kusahau!
- Ninatumia Web-Tv ninaweza kujiunga pia?
- Ndiyo, tunaruhusu japo baadhi ya watangazaji wanaweza kukataa web tv, kwa watakaokataa basi hutapokea matangazo yao. Mfumo wetu wa hisapepe.com unaruhusu watumia Web TV kujipatia pesa na mengine kama watumia kompyuta tu.
- Ninaweza kununua bidhaa kuwa kutumia salio la akaunti yangu ya hisapepe?
- Hilo ndilo lengo letu la baadaye. Kama una pesa katika akaunti ya hisapepe kwanini ishindikane kununua bidhaa kwa pesa hii? Unastahili hilo. Kwa sasa tuzingatie kwanza kupata hizo pesa na kukuza masalio yetu ya akaunti. Hakuna lisilowezekana hapa Hisapepe!
- Kwanini naulizwa namba ya simu yangu ya mkononi?
- Kwa sababu moja tu ili tukulipe malipo yako kwa njia ya muda wa maongezi “Dola” (Artime). kwenda moja kwa moja katika simu yako. Tafadhali zingatia kwamba Hisapepe.com si mtandao wa jamii ambapo marafiki hubadilishana mawazo na wasifu wao, kwa hisapepe.com kila taarifa unayojaza wakati wa kujiunga inabaki kuwa siri kati yako na hisapepe.com, wanachama wenzako ama watangazaji hawataona taarifa zako.
- Sipati ujumbe wa kufanikiwa kujiunga, kwanini?
- Baadhi ya watoa huduma wa barua pepe (email providers) kama yahoo, gmail, hotmail n.k huwa wanawakinga wateja wao na baruapepepe zinazohisiwa kuwa ni spam (spam ni baruapepe unayopokea toka kwa mtu usiyemfahamu). Kwa sababu hii barua pepe ya kwanza toka hisapepe.com inaweza isionekane, tafadhali kwanza angalia folder la SPAM/BULK/JUNK MAIL kuona kama ujumbe wako umetupiwa huko. Uzuri wa hawa watoa huduma yaani yahoo, hotmail, gmail n.k wamekupa ruhusa kukubali anayekutumia aweze kukufikia, nenda Kisha bonyeza “mark as safe” au “Not Spam” ili baruapepe toka hisapepe ziwe zinakufikia.
- Ndio nimejiunga – Inachukua muda gani kuidhinishwa?
- Kwetu hisapepe karibu kila kitu kinaendeshwa na kompyuta kwa hiyo huna haja ya kusubiri. Inapokuja kwenye suala la malipo hapo tunafanya ukaguzi wa kibinadamu kuhakiki na kisha tunakulipa mapema iwezekanavyo.
- Nimeshajiunga ila sipokei matangazo yoyote, kwanini?
- Hii inawezekana kama haupo Tanzania huenda bado hakuna tangazo linalolenga nchi yako. Pia huenda keywords ulizochagua (aina ya matangazo ya kukufikia) hazijapata mtangazaji wake tangu ujiunge. Inawezekana pia akaunti yako imesitishwa au kufutwa kabisa kwa kuwa umekiuka Masharti Ya Huduma Hii. Pia sababu nyingine inawezekana ikawa ni kwamba mtoa huduma wako wa barua pepe (email provider) kama yahoo, gmail, hotmail n.k huwa wanawakinga wateja wao na baruapepepe zinazohisiwa kuwa ni spam (spam ni baruapepe unayopokea toka kwa mtu usiyemfahamu). Kwa sababu hii barua pepe ya kwanza toka hisapepe.com inaweza isionekane, tafadhali kwanza angalia folder la SPAM/BULK/JUNK MAIL kuona kama ujumbe wako umetupiwa huko. Uzuri wa hawa watoa huduma yaani yahoo, hotmail, gmail n.k wamekupa ruhusa kukubali anayekutumia aweze kukufikia, nenda katika barua pepe yako kisha bonyeza “mark as safe” au “Not Spam” ili baruapepe toka hisapepe ziwe zinakufikia.
- Kuna namba ya huduma kwa mteja naweza kupiga ili kuwasiliana na kituo cha huduma nikitatizwa na akaunti yangu
- Karibu sana na tunapenda kukusaidia. Namba ya kupiga ni +255 715 733 833 na mhudumu wetu atakusaidia mara moja.
- Nikibadili namba yangu ya simu niliyojiunga nayo kupokelea malipo hisapepe inakuwaje?
- Una haki ya kubadili namba yako ya simu. Ukibadili nenda katika akaunti yaki ya hisapepe, ingia na kisha katika menyu yako bofya "Wasifu Wako", badili namba yako ya simu, hapo unaweza kubadili kila kilichomo isipokuwa jina la kuingilia "Username"
- Naruhusiwa kuwa na akaunti zaidi ya moja?
- Tunaruhusu akaunti moja tu kwa mwanachama mmoja. Tunaruhusu akaunti kadhaa kwa familia ila inamlazimu kila mmoja wenu awe na kompyuta yake na mtoa huduma wa internet wake yaani ISP ili awe na IP yake kushiriki katika hisapepe.
- Ninaingiaje katika akaunti yangu ya hisapepe?
- Tembelea http://www.hisapepe.com utaona sehemu ya kuingia. Weka jina ama anuani ya barua pepe naneno lako la siri kisha bonyeza ingia
- Ninashindwa kuingia, kwanini?
- Hakikisha jina lako au barua pepe ya kuingilia ni sahihi, kama umesahau bonyeza “Umesahu neno la siri?” tukutumie upya. Huwezi kuingia kama umekiuka moja ya masharti ya huduma hii, na kama umekiuka huenda akaunti yako imesimamishwa ama kufutwa..
- Akaunti yangu ya hisapepe inaisha muda wake au kufungwa baada ya muda?
- Ndiyo, tunasitisha akuanti zisizotumika kwa muda mrefu. Vilevile tunafuta barua pepe zote ulizopokea na kuziacha katika sandulu lako la hisapepe kwa siku 31 bila kuzisoma. Hata hivyo baruapepe au matangazo yaliyoytumwa kwenda katika barua pepr yako yaani yahoo, gmail, hotmail n.k HIZO HATUZIFUTI. Tunafanya hivyo kuhakikisha watangazaji wetu wanakuwa na wanachama hai.
- Kwanini akaunti yako imesimamishwa?
- Kwa sababu umekiuna Masharti yetu ya huduma hii au umekaa muda mrefu bila kuingia katika akaunti yako hivyo imesitishwa. Tunafanya hivi kwa kuwa tunataka pesa halali za wadhamini/watangazaji wetu ziende kwa wanachama wanaoweza kuwazalishia matunda ya pesa zao wanazoweka katika utangazaji/udhamini.
- Ninabadili vipi taarifa zangu nilizojaza hisapepe.com?
- Ingia katika akaunti yako, angalia sehemu ya menyu ya mwanachama utaona “Wasifu Wako” bonyeza hii kisha badili kila ukitakacho. Hutaweza kubadili jina la kuingia (username).
- Ninawezaje kusitisha upokeaji wa ujumbe/baruapepe toka hisapepe.com?
- Uanachama wako katika hisapepe.com unaturuhusu tukutumie ujumbe na matangazo ya barua pepe. Huwezi kusitisha upokeaji na bado ubaki mwanachama. Njia pekee ni kusitisha uanachama. Ingia katika akaunti yako, angalia sehemu ya menyu ya mwanachama utaona “Wasifu Wako” bonyeza hii kisha chini kabisa utaona sehemu ya kusitisha akaunti yako. Ingiza neon la siri Kisha kubali kufuta akaunti yako. Utapoteza salio/malimbikizo yote na mapato yote ungestahili kupata toka kwa uliowaalika.
- Ninasitishaje akaunti yangu?
- Ingia katika akaunti yako, angalia sehemu ya menyu ya mwanachama utaona “Wasifu Wako” bonyeza hii kisha chini kabisa utaona sehemu ya kusitisha akaunti yako. Ingiza neno la siri kisha kubali kufuta akaunti yako. Utapoteza salio/malimbikizo yote na mapato yote ungestahili kupata toka kwa uliowaalika.
- Ninapata pesa kiasi gani kwa kushiriki hisapepe?
- Kila mtangazaji/mdhamini analipa kiasi tofauti na mwenzake kwa barua pepe/tangazo/ofa n.k viwango hivi vinabadilika mara kwa mara inakuwa ngumu kutoa tamko la kiwango sahihi. Tunachofanya hisapepe.com ni kuwawekea kiwango cha chini kinachokubalika ili mwanachama ufanyapo kazi usipate hasara. Ni juu yao kuweka kikubwa ana cha ziada ila tunahakikisha haupunjiki ukizingatia unatumia muda na gharama za internet.
- Ninalipwaje?
- Malipo yanafanyika kutegemeana na hali halisi ya nchi yetu na njia za malipo zilizopo. Njia rahisi kabisa ni kukupatia Muda wa Maongezi (Airtime) yenye kiwango cha salio lako la hisapepe unaloomba kulipwa. Kuna njia za utumaji pesa kwa simu za mkononi yani Mobipawa, M-Pesa Tanzania, Z-Pesa na pia kuwekewa katika akaunti yako ya benk(kuna gharama za utumaji zitakuwa ni juu yako maana hatutozi sisi hizi gharama; (Angalia gharama hapa mobipawa.co.tz,zpesa.co.tz,vodacome.co.tz . Wanachama walio nje ya Tanzania Mnaombwa kuwa makini mnapochagua njia ya malipo. Tunashauri mchague ‘Advertising’ ambapo mtaweza kutumia salio lenu kama malipo kutangazia biashara/jambo lenu katika hisapepe.com. Paypal na njia nyingine zinakuja punde.
- Ninaweza kutoa pesa mara ngapi katika akaunti yangu?
- Hakuna idadi iliyopangwa ya wewe kutoa pesa yako, hata hivyo tunakushauri utoe kiwango kinacholeta mantiki kulingana na njia ya malipo unayotumia na gharama za utumaji kama zipo. Kiwango cha chini cha kutoa ni Tsh 1000/=.
- Kuna gharama/makato nikitaka kuchukua pesa yangu
- Malipo yanafanyika kupitia njia hizi: Muda wa Maongezi (Airtime Credit) Z-Pesa, M-Pesa-Tz, Advertising na Mobipawa. Hadi sasa utumaji wa muda wa maongezi hauna makato yoyote. Wanachama mliochagua Mobipawa, Z-Pesa, naM-Pesa kama njia zao za malipo wataingia gharama za utumaji kutegemea na huduma hizo. (Angalia gharama hizo mobipawa.co.tz. zpesa.co.tz, vodacom.co.tz (Hisapepe.com Haichukui makato/gharama hizi na haina mamlaka nazo!).
- Ninaweza kuchukua pesa yangu wakati wowote
- Ndiyo, huduma yetu ipo wazi masaa 24. Siku 7 kwa wiki!
- Ninajuaje salio langu la hisapepe?
- Ingia katika akaunti yako, kushoto kuna menyu na kuna sehemu ya "Salio Lako", bofya hii na utajua salio lako na kila kitu akaunti yako imefanya.
- Wakati gani naweza kuomba malipo?
- Mara tu akaunti yako ikishakuwa na salio la walau Tsh 1000/= unaweza kuomba kulipwa. Unaweza kuomba zote ama kiasi kadhaa katika salio lako la hisapepe.
- Ninajuaje historia ya miamala yangu (rekodi ya kazi nilizofanya na kulipwa hisapepe.com)
- Ingia katika akaunti yako, kushoto utaona "Pesa Nilizopata" fungua hii na angalia uone hisoria nzima ya akaunti yako yaani Bank Statement, utaona pesa zote ulizopoke, kutumia na kutoa, na kila kitu kinaoneshwa kwa muda sahihi uliofnya. Uwe na mazoea kujiwekea rekodi ya fedha.
- Nitaombaje Kulipwa?
- Mara tu salio lako likifikia Tsh 1000/= utaona sehemu ya kubonyeza kutoa pesa inajitokeza (‘Withdawal Request”) katika sehemu yako ya “Toa Pesa” ukishatuma ombi lako la malipo tutahakiki akaunti yako na kuanza utaratibu wa malipo. Unaweza pia kuamua badala ya kuchukua pesa ukaitumia pesa hiyo kutangaza jambo lako au biashara yako kwa wanachama wa hisapepe (redemption option) kwa punguzo maalumu.
- Inachukua muda gani kulipwa?
- Mara baada ya kuomba kulipwa na akaunti yako haina tatizo lolote tutakufanyia malipo mapema iwezekanavyo. Muda gani inachukua itategemea na idadi ya maombi ya malipo (foleni) na njia ya malipo unayoitumia. Hata hivyo kwa njia kama ya muda wa maongezi hatutarajii timu yetu ipitishe masaa 24 kabla hujalipwa.
- Nitalipwa na Akaunti zipi?
- Kamwe usiangukie mikononi mwa matapeli. Hisapepe.com haina cha kuficha inapokuja kwenye masuala ya wanachama wake. Akaunti zifuatazo tu zitatumika kukulipa wewe mwanachama (Akaunti hizi pia zinatumwa kwako kwa barua pepe mara unapojiunga)
+255 715 733 733 (tiGO)
, +255 734 733 733 (TTCL Mobile), +255 769 733 733 (Vodacom Tanzania, M-Pesa Tanzania), +255 783 333 433 (Zain Tanzania) +255 774 733 123 (Zantel Tanzania na ZPesa Tanzania +255774733733 (Zantel Tanzania, Z-Pesa Tanzania). (“733733 inasimama badala ya ‘pepe’ katika keypad ya simu yako”). Tafadhali usipige namba hizi.
Akaunti hizi zikibadilishwa tutawataarifu wanachama wote.
- Hisapepe kuna siku wataniomba niwatumie neno langu la siri?
- Hivi tulishataja hii? Hisapepe.com Hisapepe.com KAMWE HAITAKUOMBA neno la siri la akaunti yako iwe kwa njia ya barua pepe, simu ama ujumbe mfupi wa sms. Sehemu pekee utakayo hitaji neno lako la siri ni unapoingia hisapepe na pale unapotaka kubadili taarifa zako katika wasifu wako. Tafadhali tunza neno lako la siri, na usiwape wenzako hata kama ni marafiki.
- Msaasa wa Moja Kwa Moja ndio nini?
- Ukitembelea http://www.hisapepe.com/pages/swahili/contact.php utakutana na mtoa huduma kwa wateja wa hisapepe na utalonga nae moja kwa moja. Kama amebanwa sana anahudumia wateja wengine unawe kuacha ujumbe na watakujibu baadae
|
| Rudi Juu | Ukurasa Unaofuata wa Maswali>> |
|